Nojoto: Largest Storytelling Platform

Ijapokuwa ni vazi, wanawake hawavai vilemba Na hat

Ijapokuwa ni vazi, wanawake hawavai vilemba
Na hata kama inapendeza, bado hawavai kanzu
Hata kunao wengi wasopenda chupi za bambino
Nimezaliwa kikamilifu, si nusu kichotara tena ehe
Na kama kuku, napenda kula wa afya si mangisi
Niliwahi penda vidimu, ila uchachu wake uchungu
Na kila uchungu na tamule na kila tamule, tamu
Ila mhibu angu, usijigeuze chano watu watakufulia
Utamaisi fika simbuko haisimbiki ila kwa msuko
Ifanye haramu ya mchwa kuwa bidii yako tena
Ili usiishie kuomba kisiki kikukwae upate sababu
Na usije kwangu bila haja, aghalabu utanikasirisha
Maisha hayana haki kwa wanyonge, wasiojiweza
Na tajiri hata na deni, hafai kudaiwa, mkumbushe tuu.

|Maisha|
 #ushairi 
#life
Ijapokuwa ni vazi, wanawake hawavai vilemba
Na hata kama inapendeza, bado hawavai kanzu
Hata kunao wengi wasopenda chupi za bambino
Nimezaliwa kikamilifu, si nusu kichotara tena ehe
Na kama kuku, napenda kula wa afya si mangisi
Niliwahi penda vidimu, ila uchachu wake uchungu
Na kila uchungu na tamule na kila tamule, tamu
Ila mhibu angu, usijigeuze chano watu watakufulia
Utamaisi fika simbuko haisimbiki ila kwa msuko
Ifanye haramu ya mchwa kuwa bidii yako tena
Ili usiishie kuomba kisiki kikukwae upate sababu
Na usije kwangu bila haja, aghalabu utanikasirisha
Maisha hayana haki kwa wanyonge, wasiojiweza
Na tajiri hata na deni, hafai kudaiwa, mkumbushe tuu.

|Maisha|
 #ushairi 
#life
adierpalmer4947

Adier Palmer

New Creator