Urembo wako wa mbele, selfi hazifichiki Na kizingiti kwa nyuma, mwenzio hakupitiki Njoo uwe wa kwangu, huu moyo uumiliki Tubembee tukitembea, hadi sokoni Maliki Hata nyumba takujengea, iwe yako uimiliki Tupendeze walotulea, wasiseme tuu ni kiki Nikufunze nikikupea, uwe wangu 'kusadiki Mbegu ya penzi ikimea, kwangu uwe rafiki Moyo wako taujengea, ua ambalo halipitiki Na zawadi kuletea, hata kama hazifurahiki Ewe nmekupendelea, ka Chelsea na pikipiki Kwako nikajitolea, kuwa kicheko hakifichiki Ni kweli nakumezea, kwa mabusu na makiki Penzi lako limekolea, kama sukari limetiki Siko radhi kukchezea, kwako sitoki sibanduki Nataka kukupea, risasi zangu na bunduki |Mahabuba| Ewe wangu Waridi, leo tena kuna baridi. Si kidogo inazidi, na itanimaliza ikibidi... #shairi Furahia